Utangulizi

Tanzania ni maarufu kwa mamalia wakubwa katika mazingira ya aina mbalimbali. Wanyama kama tembo na simba wanawavutia watu wengi, lakini kuna aina nyingi sana za spishi za mamalia wadogo. Baadhi ya mamalia wadogo na wa pekee wanaishi Tanzania tu na wamo katika hatari kubwa ya kutoweka kabisa.

Tovuti hii imeandaliwa kwa ajili ya kuwaelimisha watu ambao siyo wataalamu wa mamalia wa Tanzania lakini wanavutiwa na viumbe hawa. Aidha tovuti hii imetayarishwa kwa ajili ya kuwasaidia wana biolojia wanaofanya utafiti juu ya mamalia wadogo na kujihusisha na uhifadhi wao.

Lengo kuu la tovuti hii ni kuwaelezea mamalia wote wa Tanzania, lakini mwanzoni tutaelezea spishi zinazopatikana kwenye milima ya Tanzania, nchi iliyopo Afrika Mashariki. Milima hii imegawanywa kwenye makundi manne makuu: milima ya kaskazini (ikijumuisha Kilimanjaro na Ngorongoro), Tao la Mashariki (ikijumuisha milima ya Usambara na Udzungwa), milima ya kusini (ikijumuisha Rungwe na Kitulo) na ufa wa Albertine (ikijumuisha Mahale). Kila kundi uasili tofauti wa kijiolojia na mifumo ya tabia ya nchi tofauti. Kuna,mamalia ambao wapo katika makundi haya yote ya milima na wengine wanapatikana kwenye kundi moja tu ya milima hii.

Tovuti hii ina taarifa zitakazokusaidia kuwatambua mamalia wa Tanzania, kuelezea kila spishi (kwa sasa tutaelezea spishi ambazo ziko kwenye kwenye maeneo yaliyopo mita 1,000 au zaidi kutoka usawa wa bahari au makundi mengine yatakayochaguliwa), muhtasari wa milima mbalimbali ya Tanzania na data zao, na vitu vitakavyotumika katika mipango ya elimu inayolenga mamalia wa Tanzania.

Tutafurahi sana kupata maoni na mapendekezo ya watu wote watakaotumia tovuti hii, ili tuweze kuiboresha. Mnaweza kuwasiliana nasi kwa kutumia anwani ya barua pepe ifuatayo: MammalsofTanzania@fieldmuseum.org

SHUKRANI NA MAREJEO

John D. na Catherine T. MacArthur Foundation na Critical Ecosystem Partnership Fund zilitoa msaada mkubwa uliogharamia utayarishaji wa Taarifa na sifa za Mamalia wa Tanzania. Mfuko wa Pamoja wa Mfumo-ikolojia unatokana na juhudi za pamoja za Shirika la Hifadhi la Kimataifa (Conservation,International), Mfuko wa Kimataifa juu ya Mazingira (Global Environmental Facility), Serikali ya Japan, MacArthur Foundation na Benki ya Dunia. Lengo kubwa la Mfuko huu ni kuhakikisha kwama makundi ya kiraia yanahusishwa katika kuhifadhi bioanuwai.,Waliohusika na utayarishaji wa Taarifa na Sifa za Mamalia wa Tanzania-,Msaada zaidi ulitolewa na John Bates, Lori Breslauer, Dana Brink, Mike Carleton, Cherry Hill Farm, Chicago Zoological Society, Amy Costello, Peter Crane, Trish DeCoster, Alison Ebert, Bill Gibson and his family, Linda Gordon, Shannon Hackett, Mary Hennon, Mary Ellen Holden, Kim Howell, Rainer,Hutterer, Sharon Jansa, Helen Kafka, Mark Kamhout, Philip Kihaule, Dieter Kock, Peter Lang, Jeremy Langdon and his family, Sarah Lansing, Richard Leakey, Tim Littig, Jim Mead, Abdoulaye Ndiaye, Debby Moskovits, David Moyer, Charles Msuya, Maiko Munissi, Phil Myers, Charlie Potter, Teresa RodriguezAlan Rodgers, Jim Schulz, Jodi Sedlock, R. Senzota, Jo Stanley, Janice Taylor, United States National Museum, Bob Weir and colleagues, Dave Willard and Don Wilson.,Picha: Rebecca Banasiak, Tim Davenport, Daniela W. De Luca, Charles Foley, Palden Hamilton, Josh Howland, Peggy McNamara, Ben Mehl, Marshall Svendsen,Tafsiri: Imani Swilla.,Wapiga picha: Rebecca Banasiak, Joe Foss, Ryan Killackey, Perry Lai, Spring Malekar, Bill Stanley, Cecily Steele, Laura Watson.,Utayarishaji wa Webu: Rebecca Banasiak, Jeremy Lane, Greg Mercer, Allyson Meyer, Rebecca Reeves, Cecily Steele.